Taharuki imetanda katika pwani ya Kenya baada ya watu watano kuuawa na
wengine kadhaa kujeruhiwa na watu waliojihami kwa silaha. Watu hao
walifyetua risasi ndani ya kanisa moja katika eneo la Likoni. Polisi
katika eneo hilo, wanasema washambuliaji waliingia kwa nguvu kanisani,
na kuwafyetulia waumini risasi. Maryam Dodo Abdalla amezungumza na Bozo
Jenje, ambaye ni mwandishi habari mjini Mombasa.
Post a Comment