Featured Post Today
print this page
Latest Post

Kombe la mataifa Afrika kitendawili



Morocco ni mwandaaji wa Michuano ya Kombe la mataifa Afrika 2015

Serikali ya ufalme wa Morocco itakutana na maafisa wa shirikisho la soka barani Afrika,CAF kwa ajili ya kufanya uamuzi kuhusu kuahirisha fainali za kombe la mataifa ya Afrika au la kwa sababu ya mlipuko wa ugonjwa wa ebola katika nchi za Afrika magharibi.
Morocco imesema haiko tayari kuandaa mashindano hayo kwa hofu ya kusambaa kwa ugonjwa huo.
CAF inataka michuano hiyo ifanyike kama ilivyopangwa ifikapo mwezi Januari na Februari mwakani.
Hata hivyo imeomba nchi nyingine saba kama wataridhia kuwa waandaaji mbadala,lakini mpaka sasa hakuna hata nchi moja iliyojibu ombi hilo.
Morocco ilipendekeza michuano iahirishwe mpaka mwezi Juni mwakani.

ManCity yaichapa Manchester United 1-0

Manchester City imeendeleza ubabe wake dhidi ya majirani zao Manchester United kwa kuwachapa goli 1-0 katika mchezo mkali uliofanyika katika uwanja wa Etihad, Jumapili.
Sergio Aguero aliipatia timu yake goli hilo katika dakika ya 63 ya mchezo.
Goli hilo la kumi kwa Aguero katika msimu huu wa ligi kuu ya England liliivunja Manchester United iliyokuwa na ngome iliyosambaratika baada ya Chris Smalling kutolewa nje kwa kadi nyekundu katika kipindi cha kwanza cha mchezo na Marcos Rojo kutolewa nje katika machela baada ya mapumziko kutokana na kuumia bega.

Chris Smalling wa Manchester United akionyeshwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Manchester City, Jumapili

Ushindi huu wa Manchester City pia unatoa mwanga wa matumaini kwa kocha Manuel Pellegrini ambaye wiki iliyopita, timu yake ilipoteza kwa West Ham katika mchezo wa ligi kuu na kisha kutolewa katika kombe la Capital One baada ya kufungwa nyumbani na Newcastle.
Manchester City walikuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo.
Mchezo kati ya Manchester City na Manchester United ulikuwa mpambano mkali, ukiwa wa kwanza kwa meneja mpya wa Manchester United, Louis van Gaal, akishuhudia ngome ya timu yake ikiyumba na nguvu ya safu ya ushambuliaji ya kina Angel Di Maria, Robin van Persie na Wayne Rooney ikishindwa kupeleka michomo iliyotarajiwa katika lango la Manchester City.

Wachezaji wa Manchester United katika moja ya mechi zao za ligi kuu ya England

Wakati meneja wa Manchester United akisikitika kwa makosa ya kizembe yaliyomsababishia Chris Smalling kutolewa nje kwa kadi nyekundu, wenyeji Manchester City walijawa na furaha kwa kushinda kwa mara ya sita katika michezo saba iliyozikutanisha timu hizo na pia Manchester City ikishinda mechi nne mfululizo dhidi ya Manchester United.
Kwa matokeo hayo Chelsea bado inashikilia usukani wa ligi kuu ya England ikiwa na pointi 26, pointi sita juu ya Manchester City na pointi nne juu ya Southampton inayoshikilia nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo.
Manchester United iko katika nafasi ya kumi baada ya michezo kumi ikiwa na pointi 13, huku Burnely ikiwa katika nafasi ya ishirini na ya mwisho katika ligi kuu hiyo, kwa kujikusanyia pointi nne tu katika michezo yake kumi iliyokwishacheza.

Hamilton amshinda Rosberg,Langa Langa

Dereva Lewis Hamilton wa timu ya Mercedes amemshinda mwenzake wa timu hiyo Nico Rosberg katika mashindano ya langa langa ya US Grand prix.
Daniel Ricciardo wa timu ya Red Bull ameshika nafasi ya tatu baada ya kuendesha vizuri dhidi ya madereva wa timu ya Williams. Kwa ushindi huo Hamilton sasa anaongoza kwa pointi 24 mbele ya Rosberg huku zikiwa zimesalia duru mbili na uwezekano kupata pointi 75 Timu ya Mercedes imetawala mashidnano ya langa langa ya mwaka huu tofauti na miaka mingine.

Rais Poroshenko apinga uchaguzi

Rais Petro Poroshenko wa Ukraine amesema kuwa hatambui uchaguzi unaoendelea katika baadhi ya maeneo ya Mashariki mwa nchi hiyo na kwamba kwa hatua hiyo wanarudisha nyuma jitihada za kuleta amani nchini humo.
Katika hotuba yake iliyoonyehswa kwenye Runinga pia Poroshenko amesema kuwa serikali yake haitatambua upigaji kura huo katuika majimbo ya Donetsk and Luhansk.
Hata hivyo amesema kuwa hali ya machafuko katika mashariki mwa taifa hilo kumesababisha kuvunjika kwa hali ya amani na kuleta vurugu.
Poroshenko amesema kuwa anataraji kupendekeza sheria itakayopiga marufuku waasi kuanzisha katika eneo ambalo limepitishwa na kuwa eneo lenye harakati za kutaka kuleta amani.

Hedhi yawa fedheha kwa wanawake India

"Sitamwaacha binti yangu ateseke kama mimi ninavyoteseka nikiwa katika siku zangu. Familia yangu inafanya nijihisi najisi.
"Siruhusiwi kwenda jikoni, Siwezi kuingia hekaluni, Siwezi kukaa na wengine."
Kuna hisia ya dhamira katika sauti ya Manju Baluni mwenye umri wa miaka 32. Nilikutana naye katika kijiji cha Uttarakhand, jimbo lenye miinuko kaskazini mwa India.
Nchini India,kuna ukimya kuhusu suala la afya ya wanawake, hususan wawapo katika siku zao. Kuna mwiko uliojikita katika jamii hizi kuhusu suala la mwanamke awapo katika hedhi: wanawake si wasafi, wachafu, wagonjwa na wakati mwingine wamelaanika katika kipindi hicho.
'Wasiwasi na Mashaka'
Watu wanaamini kuwa wanawake wanaokuwa katika hedhi hawatakiwi kuoga na wana upungufu wa damu.
Uchunguzi wa hivi karibuni wa kampuni ya kutengeneza taulo maalum za kujisitiri kina mama wanapokuwa katika hedhi umeonyesha kuwa asilimia 75% ya wanawake wanaoishi mijini bado wananua taulo hizo zikiwa zimefungwa katika mifuko au gazeti ili kutoonyesha kilichomo ndani kwa sababu ya aibu inayohusishwa na hedhi.
Mwanamke akikunja taulo za kujihifadhi wakati wa siku zake nchini India
Na kamwe hawawaombi wanaume katika familia kuwanunulia taulo hizo maalum.
Nimekulia katika nyumba yenye wanawake wengi, lakini bado hatuwezi kujadili kwa uwazi suala hili ambalo ni la kawaida.
Wasichana wanajifunza kuficha nguo zao wanazotumia wawapo kwenye hedhi kwa wanaume baada ya kuzifua, anasema Rupa Jha. Mama yangu alitumia mashuka makuu kuu na kuzificha katika sanduku, tayari kwa kutumiwa na mabinti zake wanne.
Changamoto kubwa ni namna ya kukausha vipande hivyo vya nguo. Nina kumbukumbu za kuhisi wasiwasi na mashaka juu ya mchakato mzima.
Nilifundishwa mbinu nadada zangu wakubwa - namna ya kuficha nguo zenye madoa ya damu chini ya nguo nyingine bila ya mwanaume yeyote kugundua. Hatukuthubutu kuziacha peupe kwenye jua ili zikauke kabisa.
Nilihisi 'mchafu sana'
Matokeo ni kwamba kamwe hazikukauka vizuri, ziliacha harufu ya uvundo. Nguo hizo zisizo safi zilitumika tena na tena.
Wanawake wakisikiliza mwezeshaji kuhusu hali zao za usafi nchini India
Ukosefu wa maji ulifanya kazi ya ufuaji kuwa ngumu na isiyo na usafi. Hali hiyo haijabadilika sana tangu wakati huo kwa wanawake wengi wa Kihindi.
Uchunguzi mwingi uliofanyika siku za karibuni umeonyesha kuwa mila hizi zimesababisha madhara makubwa ya kiafya. Imeripotiwa kuwa mmoja kati ya wasichana watano nchini India anaacha masomo kutokana na kadhia ya hedhi.
Baadhi ya wasichana wanaacha kwenda shule wawapo katika kipindi cha hedhi. Margdarshi mwenye umri wa miaka kumi na mitano anaishi katika kijiji cha ndani cha Uttarakashi.
Anapenda kwenda shule japo inamaanisha safari ngumu akipita katika eneo lenye vilima vikali. Kamwe hajawahi kukosa masomo, isipokuwa kwa mwaka jana wakati ambapo nusura aache masomo baada ya kupata siku zake kwa mara ya kwanza.
"Tatizo kubwa kuliko yote ilikuwa namna ya kukabiliana na hali hiyo. Bado lipo. Najisikia kufedheheshwa, hasira na mchafu sana. Mwanzoni niliacha kwenda shule."
'Suala la kibinadamu'
Anataka kuwa daktari na anashangaa kwa nini wavulana katika darasa lake wakati wa somo la elimu ya viumbe(baolojia) wanacheka sana mwalimu anapoelezea njia ya hedhi.
"Nachukia. Natamani tungekuwa huru zaidi na kujisikia huru tunapozungumzia suala hili. Hali hii inatokea kwa kila mwanamke kwa hiyo kuna nini cha kuchekesha hapo?"
Mama nchini India
Anshu Gupta, mwanzilishi wa shirika lisilo la kiserikali, Goonj, anahisi kuwa tatizo hili limejikita katika ukweli kwamba linahusishwa na wanawake.
Nchini India wanawake wanatumia taulo za kujihifadhi wakati wawapo katika siku zao kwa kutumia nguo kuu kuu. "Si suala la wanawake pekee. Ni suala la kibinadamu lakini tumelibagua. Baadhi yetu tunataka kuondokana na utamaduni huu wa kuona aibu na kunyamaza. Tunahitaji kuvunja utamaduni huu."
Shirika hili linafanya kazi katika majimbo 21 kati ya 30.
Shirika hili pia linatengeneza taulo rahisi kutokana na nguo zilizochakatwa upya ili kuwasaidia asilimia 70% ya wanawake wa India ambao hawawezi kupata taulo salama na safi.
Muhimu zaidi, wanaanza kuzungumzia suala hili. Bila kuhisi kufedheheka.
Makala ya BBC ya BBC's 100 Women yamekuwa yakitangazwa katika mtandao, katika televisheni na radio ya Idhaa ya Dunia tangu Oktoba 27-29. Changia maoni yako katika mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter, ukitumia alama #100Women.

WTC yafunguliwa rasmi jijini New York

Miaka 13 baada ya majengo ya awali ya Kituo cha Biashara cha Kimataifa, WTO kuharibiwa katika shambulio la kigaidi la Septemba 11, 2001, kituo hicho kilichopo jijini New York kimefunguliwa kwa shughuli za biashara.
Waajiriwa katika kampuni kubwa ya uchapishaji ya Conde Nast wameanza kuingia katika jengo hilo la One World Trade Centre lenye urefu wa ghorofa 104.
Kituo cha One World Trade Centre chapita majengo yote katika mtaa wa Manhattan, jijini New York
Jengo hilo lenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 3.8 limechukua muda miaka nane kulijenga na kwa sasa ndilo jengo refu kuliko yote nchini Marekani.
Limekodishwa kwa asilimia 60% na taasisi ya serikali ya Marekani ya Utawala wa Huduma imeingia mkataba wa kuchukua eneo la futi za mraba 275,000.
"Mwonekano wa angani wa jiji la New York umerejea tena," anasema Patrick Foye, mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Bandari, ambayo yanamiliki eneo hilo lililorejeshewa hali yake.
Sehemu ya kubarizi ghorofani mwa jengo la One WTC, jijini New York
Jengo hilo lenye urefu wa mita 541 kwenda juu liko katikati ya eneo hili, ikiwemo sehemu ya eneo la kumbukumbu la majengo ya zamani na makumbusho yaliyofunguliwa mwaka huu.
Eneo la kubarizi juu ya jengo hili hatimaye litakuwa wazi kwa matumizi ya umma.
Watu wakipita kando ya jengo la WTC jijini New York
Jengo hili la One World Trade Center kwa sasa linatawala anga la eneo la Manhtattan kwa kuonekana juu ya majengo mengine.
Baadhi ya watu wamezungumzia uzuri wa jengo hili.
Wafanyakazi wapatao 170 wa kampuni ya Conde Nast watakuwa wamehamia katika jengo hili wiki hii, fwakijaza ghorofa tano. Wafanyakazi wapatao 3,000 zaidi watajiunga na wenzano ifikapo mapema mwaka 2015.
Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya bandari Bwana Foye ameongeza kuwa jengo hili ndilo "jengo lenye usalama zaidi nchini Marekani".
TJ Gottesdiener wa kampuni ya Skidmore, Owings & Merrill ambayo ilitoa mchoro wa mwisho wa jengo hili amesema jengo hili limevuka mfumo wa majengo yaliyopo jijini New York na limejengwa na kuimarishwa kwa zege la chuma cha pua.
Eneo la jengo hili la One WTC pia imekodishwa kwa kampuni ya matangazo ya Kids Creative, GSA, na futi za mraba 191,000 zimekodishwa kwa kampuni ya China, ambayo inajishughulisha na masuala ya biashara na utamaduni.

Warioba adhalilishwa mdahalo wa Katiba

Katika mazingira ya kutatanisha, siku ya Jumapili vurugu zimekatisha mdahalo uliokuwa ukiendelea kujadili mchakato wa katiba mpya ya Tanzania huku baadhi ya watu wakipigwa na kujeruhiwa.
Mdahalo huo uliokuwa ukitangazwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni ulivurugika kutokana na kundi la vijana wapatao 20 kuanza kumzomea aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, alipokuwa akiwasilisha mada yake.
Vijana hao ambao haijajulikana walitokea wapi au walikuwa na ajenda gani waliinua mabango ya kupinga msimamo wa waliokuwa wakiendesha mdahalo na kusema rasimu ya katiba iliyopendekezwa inakidhi mahitaji yote na kusema hakuna haja ya mdahalo.
Jaji Warioba ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania alifanikiwa kutoka nje ya ukumbi ulipokuwa ukifanyika mdahalo huo mjini Dar Es Salaam, lakini wapo watu waliojeruhiwa kutokana na kurushwa viti na vitu vingine.
BBC iliwasiliana na Jaji Warioba apate kueleza yaliyotokea na kama yuko salama baada ya vurugu hizo, lakini aliomba radhi kwa kusema hayupo tayari kulizungumzia swala hilo.
Kiongozi wa kitengo cha hamasa umoja wa vijana CCM (UVCCM), Paul Makonda, aliyekuwepo ukumbini alidaiwa kuhusika na vurugu. Lakini alipoulizwa na BBC kujibu tuhuma hizo Bw Makonda amekanusha kuhusika nazo huku akisema kwamba alihudhuria mdahalo kwasababu ulikuwa wazi kwa kila mtu.
Wakati wa vikao vya Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma, Makonda aliwahi kutoa kauli za kumkebehi Jaji Warioba ambaye tume yake iliandaa rasimu ya iliyokuwa ikijadiliwa na bunge hilo.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, aliieleza BBC kuwa hana maelezo ya kutosha na kwamba atalizungumzia akipata taarifa rasmi ya kiofisi.
Tanzania ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya. Rasimu iliyodaliwa na kupitishwa na bunge lililosusiwa na vyama vya upinzani inatarajiwa kupigiwa kura na wananchi mwezi Aprili, 2015.
Wachambuzi wa maswala ya kisiasa wameeleza wasi wasi kuwa endapo hakutakuwa na kuvumiliana hali ya kisiasa nchini humo inaweza kubadilika na kuleta ghasia ambazo zinaweza kuepukika.

What Causes Saggy Breasts?

What Causes Saggy Breasts?

StockbyteGettyLatch.jpg - Stockbyte/Getty Images

Number of Pregnancies: The more children you have, the more stretched your breasts will become.

Breast Size and Shape: Smaller breasts with a rounder bottom tend to hold their shape better than larger or narrow breasts.

Weight Gain: Additional weight may lead to larger, stretched out breasts.

Smoking: Smoking causes the skin to lose elasticity, so smokers are more likely to develop sagging.

Genetics: The genes you get from your family will play a part in the size and shape or your breasts, the strength of your Cooper's ligaments, and your body weight.

Age: Regardless of pregnancy and breastfeeding, age will eventually catch up with every woman. Unfortunately, sagging is a just a normal part of the aging process.

MAKOSA 10 HATARISHI YA MATUTIMIZI YA KONDOMU

Makosa 10 Hatarishi ya Matumizi mabaya ya Kondom Usiyoyatilia mkazo

1. Kutoangalia kama imeharibika

Watu wengi hutoa kondom na kuivaa pasipo kuangalia kama kuna matundu yanayo onekana kwa macho au haipo katika halia nzuri.

2. Kutokuangalia kama imeisha muda wa matumizi(expire date).

Kati ya asilimia 61 ya watumiaji wa kondom hawana muda wa kuangalia kama zimeisha muda, kutokana na ukweli kwamba hata anapopewa huificha haraka kwa kuichimbia mfukoni na kuifungua wakati wa tukio.

3. Kutojadiri na mwenza wako matumizi ya kondom kabla ya tendo.

watumiaji wengi wa kondom hawajadiri, matumizi ya kondo badala yake inakua kikwazo pale muhusika mmoja wapo atapotoa sharti la kutumia. hii itapeleka kondom kutotumika ipasavyo sababu ya kutoridhiana matumizi yake kabla. Mshiriki mmoja anaweza kufanya ujanja hata wa kuitoboa labda kwa kuhisi amelazimishwa kuitumia bila ridhaa na kutopata raha aliyohitarajia. Jadiri matumiz mazuri ya kondom kabla ya tendo na mwenza wako na mridhiane

4. Kuchelewa kuvaa kondom.

Watu wengi hupenda kujifanya wamesahau kondom na kujikuta wakitaka kuingiliana kidogo na baadae kuvaa kondom wakiamini kua ile mara ya kwanza haina madhara, jua kwamba hata muingiliano mdogo tu waweza leta madhara kama mimba na magonjwa ya ziana sababu ya maji maji ya mwanzoni yanayotoka kutokana na matamanio ya kingono.

5.Kutokuacha nafasi wakati unapo ivaa.

watu 7 kati ya 10 hawaachi nafasi wanapo vaa kondom hii inapelekea kutojua kuwa uachaji nafasi usaidia kondom isipasuke na pia shahawa zipate nafasi ya kujilundika ili zisije kutokea mwishoni mwa pindo shinani.

6. Kuvaa ndivyo sivyo

Asilimia kubwa sana ya watu huvaa kondom nje ndani au kuigeuza, hii pia ni hatari iwapo itakua ni mara ya pili baada ya tendo kupelekea kujigusisha maji ya mwanaume na kuhatarisha tendo zima kutokua salama, hakikisha unaiangalia vzr kabla ya kuivaa nakujua nje ni wapi na ndani ni wapi.

7. Kondom kupasuka

Asilimia 29 za watu huripoti kondom kupasuka, hii inatokana na kutojua kuitumia vizuri na makubariano baina ya wenza.

8. kondom kutoka wakati wa tendo

hii hutokana na kondo kutovaliwa vizri na mtumiaji kutojua aina ya kondom inayo mkaa vyema. kama unahitaji usalama wa kula vizuri lazima ujue radha ya chakula chako, jua aina ya kondom inayokutosha vyema na upo na ustadi wa kuitumia.

9.Kuwahi kutoa kondom

asilimia 13 ya wanaume wameripoti kutoa kondom mara tu wamalizapo tendo, na kupelekea wenza wao kupata mimba au maambukizi ya zinaa, malalamishi ya asilimia 11 ya wanawake kupata magonjwa na zinaa au mimba yameripotiwa wakati wenza wao wametumia kondom. hii inatoka nakujipakaza maji maji ya mwisho yanayokua yanaishia na matumiz ya kutojua ya kondom.

10. Kutovaa kabisa kondom

Aslimia kubwa sasa ya vijana kwa wazee wamekua na kujidanganya kua maambukiz makubwa ni kutokojolea kwenye uke wa mwanamke, lakinin kumbuka kitendo hichi kinamsisimko unao weza kukufanya ushindwe kumudu kutoa kwa haraka, pia kuna kutoa maji maji ya mwanzon ambayo husababishwa na muhemuko wa kingono.... baki salama tumia kondom kwa uhakika na acha michepuko

Washambuliaji kanisa Kenya wasakwa

Taharuki imetanda katika pwani ya Kenya baada ya watu watano kuuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa na watu waliojihami kwa silaha. Watu hao walifyetua risasi ndani ya kanisa moja katika eneo la Likoni. Polisi katika eneo hilo, wanasema washambuliaji waliingia kwa nguvu kanisani, na kuwafyetulia waumini risasi. Maryam Dodo Abdalla amezungumza na Bozo Jenje, ambaye ni mwandishi habari mjini Mombasa.
 
Support : | |
Copyright © 2011. JAMII MIXER - All Rights Reserved
Published by S.M