Mbunge agawa kompyuta 28 jimboni kwake

Mbunge agawa kompyuta 28 jimboni kwake

Jituson ambaye ni Mwanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa huo, (Mamec) alisema alitoa kompyuta mbili mpakato (Laptop) kwa ajili ya waandishi wa habari wa mkoa huo, ili waweze kuandika habari za vijijini.

Babati. Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, mkoani Manyara, Vrajilal Jituson kupitia Mfuko wa Ofisi yake ameazimia kutoa kompyuta mpakato 28 kwenye maeneo tofauti ya jimbo lake kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi wa taasisi mbalimbali.
Jituson ambaye ni Mwanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa huo, (Mamec) alisema alitoa kompyuta mbili mpakato (Laptop) kwa ajili ya waandishi wa habari wa mkoa huo, ili waweze kuandika habari za vijijini.
Akizungumza jana mjini Babati, mbele ya Rais wa Muungano wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Keneth Simbaya, mbunge huyo alisema amejitolea kompyuta hizo kwa lengo la kurahisisha teknolojia ya mawasiliano.
“Pamoja na kuwapa waandishi wa habari hizo laptop mbili pia tumetoa laptop mbilimbili kwenye vituo vya polisi vya mjini Babati na Magugu ili waweze kusaidia jamii kuandika taarifa zao,” alisema Jituson.
Alisema katika kompyuta hizo 28, amepanga kugawa kompyuta tano kwa kila tarafa ili zipelekwe kwenye shule za sekondari, kwani lengo lake ni kila shule ya sekondari katika kata ipate kompyuta yake.
Kwa upande wake, Simbaya alipongeza hatua ya mbunge huyo kugawa kompyuta hizo kwa waandishi wa habari kwani amekuwa tofauti na wabunge ambao wanawathamini waandishi kwenye kipindi cha uchaguzi pekee.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : | |
Copyright © 2011. JAMII MIXER - All Rights Reserved
Published by S.M